Energy and climate change post 2015-Youth envisioning towards sustainable development

AD (728x90)

Powered by Blogger.

Blog Archive

Wednesday, October 2, 2013

press release

Share it Please
Baraza Kuu Kivuli La Umoja wa mataifa la Kanda ya Afrika Mashariki (EARMUN) ni mfano wa Baraza Kuu La Umoja Wa Mataifa ambapo vijana kati ya umri wa miaka 18 hadi 35 kutoka maeneo mbalimbali ya Afrika Mashsariki kama Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudan ya kusini, Jamhuri ya Kongo, Zambia, Ethiopia pamoja na nchi nyingine za Afrika hupata fursa ya kufanya kazi kama wanadiplomasia; hufanya utafiti wa masuala ya kimataifa; hujadili; huelimishana; hushauriana na hatimaye Kuja na  masuluhisho ya matatizo mbalimbali ya dunia.


Mwaka huu mkutano huu utafanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo Dar es Salaam Tanzania kuanzia tarehe 06 mpaka12 mwezi Oktoba 2013 ikiwa na kichwa kikuu cha, "Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi:– Maono ya Vijana kuelekea maendeleo endelevu baada ya 2015" Lengo kuu la mkutano huu ni kujadili masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia nchi na madhara yake katika nchi zinazoendelea na hasa kupendekeza njia bora ya kuokoa hali hiyo. 


Mgeni rasmi katika mkutano huu atakua Mh. Prof. Sospeter Muhongo, Waziri wa Nishati na Madini Tanzania.
Majadiliano haya yamelengwa ili kuwawezesha vijana kupata taarifa za kina juu ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi, kujadili masuala muhimu yanazunguka Nishati na Tabia Nchi duniani kote. Mkutano huo pia una lengo la kuchangia kwenye mijadala inayoendelea ya Ajenda za baada ya 2015 ya Dunia tunayoitaka.
Tangu mwaka 2006 Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa ya Tanzania, Asasi ya Umoja wa Mataifa ya Kenya, Asasi ya Umoja wa Mataifa ya Uganda, tumekua tukiandaa
Baraza Kuu Kivuli La Kimataifa la Kanda ya Afrika Mashariki kwa ajili ya vijana kila mwaka. Mikutano hii huwa ina lengo kuu la kushirikisha vijana katika majadiliano ya Malengo ya Maendeleo ya Kimilenia.
Mkutano wa mwaka huu imekuwa kufadhiliwa na Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje; Ubalozi wa Norway; Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa;. Tunatumia fursa hii kuwaomba vijana wote wa Afrika ya Mashariki pamoja na jamii kujiunga na vijana wanapokutana katika majadiliano haya ya Malengo ya Maendeleo ya Kimilenia. Pia tunachukua nafasi hii kuwaomba mashirika ya serikali na yasiyo ya serikali kuungana mikono na vijana wanaposhiriki katika fursa hii pekee inayolenga kuleta vijana wa Tanzania karibu zaidi na Umoja wa Mataifa na vilevile kwa ulimwengu.
Imetolewa na
Mratibu Mkuu

Baraza Kuu Kivuli La Kimataifa la Kanda ya Afrika Mashariki

0 comments:

Post a Comment

© 2013 EARMUN2013. All rights resevered. Designed by Templateism